product.title

Module 5 - Kutafsiri Biblia

Kulingana na ushahidi wa wazi wa maandiko yenyewe, Mungu huwaandaa wawakilishi wake kupitia Neno la Mungu lililopuliziwa na Roho, Maandiko. Kila mtu ambaye Mungu anamwita katika huduma lazima adhamirie kujinidhamisha ili aweze kuwa mahiri katika Neno, kutii maagizo ya Neno, na kufundisha kweli ya Neno la Mungu. Kama mtenda kazi, lazima ajitahidi kutumia kwa halali Neno la kweli, na hivyo kukubaliwa na Bwana katika jitihada zake za kujifunza (2 Tim. 2:15).

Katika kozi hii tunaangazia hitaji la ufasiri wa kibiblia, na kile kinachohitajika ili kutekeleza kazi hii kuu. Tutachunguza viwango vya kimungu na vya kibinadamu vya Biblia, na kutambulisha mbinu mwafaka ya ufasiri wa kibiblia iliyoundwa ili kukusaidia katika jitihada zako za kujifunza Maandiko ili kuziba pengo kati ya ulimwengu wa kale na wa sasa. Zaidi ya hayo, tutaangazia umuhimu wa aina za fasihi katika ufasiri wa Biblia, na kuchunguza aina nyingi za zana thabiti za marejeo za kitaaluma tunazoweza kuzipata tunapojaribu kuelewa maana ya Maandiko ya Biblia.